MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Feb 22, 2014

BASIC ICT SKILLS AND ICT INTEGRATION IN EDUCATION SCIENCE AND MATHEMATICS SECONDARY SCHOOL TEACHERS

 walimu walio hudhuria mafunzo ya ICT wakiwa darasani 

 walimu wakiwa katika mtihani wa mafunzo ya ICT chuo kikuu huria tawi la mwanza


 mkufunzi wa mafunzo ya ICT Bw. Mnyanyi akiwapa elimu walimu waliohudhuria mafunzo ya ICT

 wakiwa darasani kwa umakini zaidi wakisikiliza somo kutoka kwa mwalimu wao 


 wakiwa katika mjadala baada ya mafunzo na hapo aliwauliza swali  waliuliza swali 

 Madam Stella ambaye ni mwalimu wa shule ya sekondari  akijibu swali darasani huyu ni muwakilishi toka wilaya ya sengerema ni miongoni mwa walimu waliohudhuria mafunzo ya BASIC ICT SKILLS


 wakufunzi wa mafunzo ya Basic ICT Skills wakizungumza na walimu walio hudhuria mafunzo ya ICT
jijini mwanza


 mmoja wa walimu aliyehudhuria mafunzo hayo akitunukiwa cheti na wakufunzi wa mafunzo 


 akiwa na furaha tele baada ya kutunukiwa cheti cha mafunzo ya Basic ICT Skills


 wahitimu wa mafunzo ya Basic ICTskills wakionyesha vyeti vyao baada ya kutunukiwa na chuo kikuu huria cha Tanzaia { The open University of Tanzaia}

walimu hao wa shule za sekondari wakionyesha tabasamu na sura zenye kujawa furaha baada ya kuhitimu mafunzo ya BASIC ICT SKILLS 


 Mwalimu Nestory Ligembe amabye pia nae alipata fursa ya kuzungumza na walimu hao walio hudhuria mafunzo ya Basic ICT skills katika chuo kikuu huria cha Tanzania tawi la mwanza alipata kuongea nao na kuwapa nasaha zaidi juu ya masuala yanayolenga maisha ya Elimu zaidi.

 walimu wakiwa katika furaha wakielekea kupiga picha ya pamoja nje ya jengo la PPF PLAZA jijini mwanza ambapo ndipo kilipo chuo kikuu huria cha Tanzania 



 picha ya pamoja ya walimu waliohudhuria mafunzo ya BASIC ICT SKILLS 



kutoka kushoto ni muwakilishi wa walimu waliohudhuria mafunzo na akifatiwa na mratibu wa mafunzo Bw, BENJAMIN BUSSU, akifatia Mwl, Nestor Ligembe, mwisho ni mkufunzi wa mafunzo Bw, Mnyanyi
wakiwa katika picha ya pamoja nje ya jengo la PPF PLAZA MWANZA

Na wambura Mwikwabe,

Chuo kikuu huria cha tanzania. {The Open University Of Tanzania} kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya ufundi  Tanzania, wametoa kipumbele kwa walimu wa shule za sekondari kitengo cha masomo ya sayansi na hesabu kwa lengo la kukuza mustakabali wa teknolojia ya mwanzo, baadhi ya walimu hapa nchini Tanzania kupitia mpango wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wamepata fursa ya kujiunga na mafunzo yatolewayo na chuo hiki huria cha Tanzania, ambapo mafunzo hayo yamechukua takribani wiki mbili Tangu Tarehe 10 /02/2014 Hadi Trehe 22/02/2014. mkoa wa Mwanzam,  kwa kanda ya ziwa wamechukua baadhi ya walimu kutoka baadhi ya wilaya kama vile Geita Bukombe Chato, Sengerema,  na pia hata Mkoa kagera pia nao wamepata fursa hii na pia zoezi hili limejuisha mikoa yote ya Tanzania. kwa lengo la kukuza teknolojia na kupeana taarifa zaidi juu ya sayansi na teknolojia haya habari na mwasiliano, hivyo basi baadhi ya wahitmu hao wametunukiwa vyeti vya mafunzo ya BASIC ICT SKILLS.
zoezi hili bado linaendelea katika mikoa mingine kama kawaida.

PICHA ZOTE KWA HISANI YA CHUO KIKUU HURIA KITENGO CHA MAFUNZO YA KOMPYUTA  TAWI LA MWANZA.

THE OPEN UNIVERSITY OF TANZANIA
INSTITUTE OF EDUCATION AND MANAGEMENT TECHNOLOGY
MWANZA REGIONAL CENTER
 PPF PLAZA TOWER
4th floor and 5th floor
+255756185684/ +255754766910
www.out.ac.tz