MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Dec 14, 2014

Jenerali aliyempinga Museveni arudi UG


 Jenerali Sejusa aliyeitoroka uagnda baada ya kutofautiana na rais Musevenei hadharani 

Mwanajeshi wa Uganda ambaye alitofautiana hadharani na rais wa nchi hiyo Yoweri Museveni mwaka uliopita amerejea nchini Uganda bila kutarajiwa kutoka nchini Uingereza ambapo alikuwa amekimbilia uhamishoni.
Jenerali David Sejusa aliitoroka Uganda baada ya kumshutumu rais Museveni kwa kujaribu kubuni familia ya kifalme akitaka kumkabidhi uongozi mwanawe wa kiume.
Sejusa pia alidai kuwa kulikuwa na njama ya kuwaua watu fulani katika serikali na jeshini ambao walikuwa wakipinga mpango huo.

Alipowasili mjini kampala Jenerali Sejuse alikutana na mkuu wa ujajusi ambapo pia aliwaambia waandishi wa habari kuwa rais Museveni alifahamu kuhusu kurejea kwake.