Dereva Jenson Button, wa timu ya McLaren, anamatumaini ya kuendelea kuitumikia timu hiyo zaidi.
Jenson
Button, amesaini mkataba wa miaka miwili utakaomuweka na timu hiyo
mpaka 2016.Button amechaguliwa kuwa timu moja na nyota Fernando Alonso.
"kuwa na timu ya Mclaren, kwa Zaidi ya mwaka mmoja ni muhimu ,ila niko
hapa kwa ajili kupamba na michuano ya dunia” Button mwenye miaka 34
awali alionyesha kuchanganyikiwa na ucheleweshwaji wa kutatua
mustakabali wake katika timu Mclaren. Mwenyekiti Ron Dennis, ameeleza
ilichukua muda kuamua kati ya Button, na mchezaji mwenzake Kevin
Magnussen, nani atashirikiana na Alonso, ila ikafikiwa muafaka kwa
Button kuchaguliwa. Timu ya McLaren imewatangaza Jenson Button ,Fernando
Alonso na Kevin Magnussen kuwa madereva wa timu hiyo kwa msimu ujao wa
mwaka 2015.