Sep Blatter
Shirikisho la mpira wa miguu
duniani Fifa wiki ijayo watapiga kura ili kuamua kuwekwa hadharani kwa
ripoti ya uchunguzi wa mgogoro wa rushwa katika utoaji zabuni za kuandaa
michuano ya kombe la dunia la mwaka 2018 na 2022. Mkutano huu utakao
fanyika jijini Marrakesh nchi morocco utatoa maamuzi ya kuweza
kusambazwa ripoti ya uchunguzi wa kashfa ya rushwa katika kutoa nafasi
ya wenyeji wa michuano ya kombe la dunia. Viongozi wa soka chini ya
mapendekezo ya kamati ya maadili ya Fifa ilisisitiza sio rahisi kutolewa
kwa ripoti hiyo kwa sababu za kisheria. Fifa wamewapa nafasi Urusi kuwa
wenyeji wa kombe la dunia mwaka 2018 na Qatar kwa mwaka 2022,Uteuzi wa
nchi hizi unaonekana umegubikwa na mazingira ya rushwa.