MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Mar 6, 2015

Faiza na Wenzake Watoa Msaada wa Kuboresha Vyoo Shule ya Msingi ya Mwnanyamala Kisiwan

 Faiza Ally katikati akiwa ameshika sink la choo tayari kwa msaaa wa shule 

Mwigizaji wa filamu na  Faiza Ally siku ya jana akiwa na wenzake walitoa msaada wa vifaa vya kujengea  vyoo bora kwenye shule ya msingi ya Mwananyamala Kisiwani iliyopo jijini Dar.
“Tumefurahi tumefanikiwa tulijichangisha tukaweza kununua vyoo 10 kwa ajili ya kusaidia watoto wa shule ya mwananyamala kisiwani- ninajisikia very proud na team yangu”-


Faiza aliandika mtandaoni mara baada ya kubandika picha hizo hapo juu wakiwa shuleni hapo.
“Watoto wamefurahi  final wataingia kwenye vyoo visafi na salama”-Faiza aliandika akiwa pamoja na watoto hao.
Pia Faiza aliwashukuru watu wengi ambao walimpongeza na kumpa moyo na kuahidi kuwa ataendelea kufanya hivyo.
“Asanteni wote kwa pongezi zenu - comment zenu ni zuri kwetu maana zinatupa moyo wa kufanya tena na tena Insha Allah”
Bongomovies.com pia inakupongeza kwa moyo wako wakusaidia jamii, ni mfano mzuri umeuonyesha  ukiwa kama kioo cha jamii, Mungu akuongezee pale palipopungua.