MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Mar 9, 2015

Wimbo wa “Ntampata Wapi”, Diamond Hakuniimbia Mimi- Wema Sepetu

Mrembo na staa wa Bongo Movies, Wema Sepetu ametoboa kuwa wimbo wa “Ntampata Wapi” ulioimbwa na aliekuwa mpezi wake, Diamond Platnumz hakuimbiwa yeye, hii ni kutokana na watu  wengi kudhani kuwa  wimbo huu alitungiwa yeye ukizingatia kuwa  wakati wimbo huo unatoka ndio kilikuwa kipindi wametoka kuachana.

 “Leo nasema rasmi kuwa hii nyimbo hakuniandikia mimi….because nilikuwa naisikia hii nyimbo hata wakati tulipokuwa kwenye uhusiano amekuwa akiimba, akiindika kwahiyo ilikuwa tu ni moja ya nyimbo zake kama anavyoandika nyimbo zote lakini nadhani tu timing ya kutoka ndio kidogo imekuwa na utata because kaitoa timing ambayo watu wote wakadhani kamuimbia Wema but in real sense noo,” aliongeza Wema.
Wema ameyasema hayo hivi majuzi alipokuwa jijini Arusha  wakati akifanya mahojiano na kituo cha redio cha Radio 5 cha jijini humo.