Pichani
ni baadhi ya wakazi wa maeneo mbali mbali ya jiji la Dar, wakiwa kwenye
foleni ya kununua umeme wa luku kwenye kituo cha Sayansi, Kijitonyama
baada ya kupatwa na kwikwi kwa siku kadhaa zilizopita kwenye vituo
vingine pamoja na kwenye mitandao ya simu.ila sasa Tanesco wametoa
taarifa na kusema mambo yako mswano kwa sasa.
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA (TANESCO)
TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA LUKU KWA BAADHI YA MAWAKALA
Shirika
la Umeme Tanzania (TANESCO) linatoa ufafanuzi juu ya tatizo
lililojitokeza kwa baadhi ya mawakala wa LUKU kushindwa kutoa huduma ya
kuuza umeme. Hali hiyo inatokana na Kampuni ya Selcom ambaye ni wakala
wa kuuza na kuyaunganisha baadhi ya makampuni ya simu kwa Tanesco
kusitishiwa huduma kutokana na kushindwa kutekeleza baadhi ya majukumu
yake kimkataba.
Wakati
suala hili likiendelea kushughulikiwa na mamlaka zinazohusika tunapenda
kuwahakikishia wateja wetu kuwa, huduma zinaendelea kupatikana kupitia
Kampuni ya MAXCOM katika Vituo mbalimbali, ATM za CRDB na NMB, NMB
Mobile pamoja na ofisi zote za Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) nchi
nzima hadi siku ya Jumamosi na Jumapili na siku za Sikukukuu kuanzia saa
2:00 asubuhi hadi saa 2:00 usiku.
Shirika linaomba radhi kwa usumbufu wowote unaojitokeza.
Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano
TANESCO Makao Makuu.