Meya wa mji wa Baltimore nchini
Marekani Stephanie Rawlings-Blake, anasema kuwa amehusunishwa na
kuvunjwa moyo baada ya polisi sita kushtakiwa, kufuatia kifo cha
mwananamme mweusi Freddie Gray.
Polisi mmoja anakabiliwa na
mashtaka ya mauaji huku wengine watano wakikabiliwa na mashtaka ya kuua
bila kukusudia na kukamata kuliko kinyume cha sheria.Tangazo hilo lilisababisha watu kusherehekea kwenye mji wa Baltimore lakini wengine hata hivyo waliiendelea kuandamana.
Wakili anayewakilisha chama cha polisi katika mji huo, alilaani kile alichokitaja kuwa kuharakisha katika kuwafungulia mashtaka polisi hao.
Rais wa Marekani Barack Obama anasema kuwa, ni muhimu uchunguzi kubainisha ukweli kuhusu kile kilichosababisha kifo cha bwana Gray.
na bbc