Ripoti kutoka kaskazini mwa Syria
zinasema kuwa zaidi ya raia 50 wameuawa kwenye shambulizi la angani
lililoendeshwa na muungano unaongozwa na Marekani.
Shirika la haki
za binadamu lenye makao yake nchini Uingereza linasema kuwa kijiji
kinachofahamika kama Birmahle kilishambuliwa na kuwa bado watu wamekwama
kwenye vifusi.Muungano huo unaoongozwa na Marekani haujatoa tamko lolote kuhusu kisa hicho kufikia sasa.