MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Sep 12, 2015

MSIKITI NCHINI SAUDI ARABIA WAPOROMOKA NA KUUA WATU 107

Kreni  baada ya kuangukia msikiti wa Masjid al-Haram
Uokoaji ukiendelea
Waumini wa dini ya kiislam wakitaharuki msikitini hapo mara baada ya tukio hilo. Waokoaji Hali ilivyokuwa ndani ya msikiti wa Masjid al-Haram. Jengo lilivyoporomoka.Msikiti wa Masjid al-HaramMasalia baada ya jengo kuporomoka.
Mecca, Saudi Arabia
Upepo mkali umeukumba msikiti mkubwa zaidi dunia wa Masjid al-Haram uliopo katika Mji wa Mecca nchini Saudi Arabia na kuua watu wapatao 107 huku wengine 238 wakiwa majeruhi.
Tukio hilo lilitokea jana ijumaa majira ya mchana baada ya upepo huo mkali uliokuwa ukivuma kwa kasi ya ajabu kuikumba kreni ya mizigo iliyokuwa ikitumika kwa ujenzi juu kabisa ya ghorofa la msikiti wa Masjid al-Haram.
Baada ya upepo kuikumba kreni iliangukia kwenye msikiti hivyo kuporomosha msikiti huo na kusababisha vifo vya watu 107 na maafa mengine zaidi.
Gavana katika Mji wa Mecca ameamrisha kufanyika uchunguzi kufuatia tukio hilo.
Mkuu wa idara ya ulinzi wa angani nchini humo alisema kuwa, kulikuwa na mvua kubwa wakati ajali hiyo ilipotokea na upepo ulikuwa ukivuma kwa mwendokasi wa takriban kilomita 83 kwa saa. Msikiti huo unazunguka eneo takatifu la kiislamu la Kaaba na ndio msikiti mkubwa zaidi duniani na huwavutia mamia ya waislamu ambao huenda kuhiji kila mwaka. Karibu watu milioni moja wamewasili nchini Saudi Arabia kabla ya sherehe za mwaka huu ambazo zinaanza wiki mbili zijazo.
CHANZO: BBC NA CNN