MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Sep 11, 2015

WARIOBA, WASIRA NA LIGORA WAMMWAGIA SIFA DK MAGUFULI

 Mgombea urais kupitia CCM, Dk John Magufuli akiwapungia mkono wananchi kuwaaga baada ya kumaliza kufanya kampeni kwenye Uwanja wa Sabasaba, wilayani Bunda, Mara jana

 Watu wakiwa wamefurika kumsikiliza Dk Magufuli akijinadi katika Mji wa Nyamswa, Bunda Vijijini ambapo ameahidi kukamilisha ujenzi wa Barabara ya lami inayotoka Bunda  kwenda Nyamuswa hadi Musoma.
 Dk Magufuli akihutubia wananchi na kuomba kupigiwa kura  siku ya uchaguzi mkuu Oktoba 25 mwaka huu
 Waendesha Bodaboda wakiwa msikiliza kwa makini Dk Magufuli mjini Bunda
 Dk Magufuli akiwanadi wagombea ubunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Steven Wassira (kushoto) na Ligora wa Jimbo la Mwibara. Ligora alimmwagia sifa lukuki Dk Magufuli kuwa ndiye chaguo la Mungu kuiongoza nchi hii  kuliko wagombea wengine 7.
 Mgombea ubunge Jimbo la Mwibara, Kangi Ligora akinadiwa na Dk Magufuli
 Steven Wassira anayewania Jimbo la Bunda Mjini, akinadiwa kwa wananchi
 MMadiwani wa Kata za Jimbo la Bunda Mjini kupitia CCM wakinadiwa kwa wananchi
 Wassira hoyeeeeeeeeeeee
 Alitekuwa Katibu Mwenezi wa Chadema, Emmanuel Malima akitangaza rasmi kukihama chama hicho na kujiunga na CCM baada ya kukerwa na kitendo cha  Mgombea wao  wa Ubunge aliyeshinda kura za maoni kukatwa na kuwekwa  Esther Bulkaya aliyehamia chama hicho kutoka CCM, zaidi ya wanachama wa Chadema 120 wameamua kukimbia chama hicho
 Mmmoja wa wanachama wapya wa CCM walioihama ChademaMjini Bunda
 Aliyeshinda kura za maoni za kuwania ubunge kupitia Chadema na kukatwa jina lake akitangaza kuhamia CCM Mjini Bunda
 Dk Magufuli akiwaaga wananchi mjini Bunda
 Dk Magufuli akishauriana jambo na Jaji mstaafu Joseph Warioba (katikati) pamoja na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, Abdallah Bulembo katika mkutano wa kampeni katika Mji wa Nyamswa, Bunda Vijijini
 Jaji mstaafu Joseph Warioba akitangaza wasifu wa Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk Magufuli na kwamba anafaa kuwa rais wa Tanzania tofauti na wagombea wengine saba. Amesema kuwa sifa alizonazo zinafanana na za Baba wa Taifa, marehemu Julius Nyerere. Warioba ni mzaliwa wa Nyamuswa.
 Makongoro Nyerere ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya kampeni ya CCM, akimuombea kura Dk Magufuli katika mkutano wa kampeni mjini Nyamuswa
Wananchi wakikubali kumpigia kura zote Dk Magufuli pamoja na Mbunge na madiwa wa chama hicho
Dk. Magufuli ameahidi kujenga barabara za lami na kutatua taitizo la maji wilayani humo, atakaposhinda urais Oktoba 25 mwaka huu.
PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA WA MATUKIO BLOG