MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Nov 23, 2015

MAZISHI YA MAWAZO BADO KIZUNGUMKUTI. CHADEMA KUTINGA MAHAKAMANI.

Na:George Binagi-GB Pazzo @BMG
Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kimesitisha shughuli za mazishi ya aliekuwa Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoani Geita marehemu Alphonce Mawazo, baada ya jeshi la polisi Mkoani Mwanza kuzuia zoezi la kuuaga mwili wake lililokuwa limepangwa kufanyika juzi jumamosi Jijini Mwanza. 

Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa, Freeman Mbowe alibainisha hayo jana wakati akizungumza na Wanahabari Mkoani Mwanza, ili kutoa msimamo wa Chama baada ya kuwepo kwa mazungumzo baina yake na familia ya marehemu Mawazo. 

Alisema kuwa baada ya mazungumzo hayo, Chadema pamoja na familia ya marehemu Mawazo wamekubaliana kwenda Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza kufungua shauri la kuomba tafsiri ya Kimahakama juu ya zuio hilo la jeshi la polisi kuzuia mwili wa marehemu Mawazo kuagwa Jijini Mwanza kabla ya Kwenda kuzikwa Kijijini kwake Chikobe katika Wilaya ya Busanda Mkoani Geita.

Nae Mchungaji Charles Lugiko ambae ni baba mlezi wa marehemu Mawazo, alisema anasikitishwa na hatua iliyochukuliwa na jeshi la polisi ya kuzuia mwili wa marehemu Mawazo kuagwa Jijini Mwanza ambapo ameeleza kuwa na matumaini makubwa ya kwamba mahakama itatenda haki juu ya suala hilo.

Frederick Sumaye pamoja na Edward Lowasa ambao ni Viongozi Waandamizi wa Chadema, walisema hatua ya jeshi la polisi kuzuia mwili wa Mawazo kuagwa Jijini Mwanza si sawa na kwamba inaweza kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani.