Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi aliyeteuliwa hivi karibuni,
John Mngodo, akijitambulisha kwa Watumishi
mara baada ya kuanza kazi rasmi
katika Wizara hiyo. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa
Rasilimali Watu, Lilian Mapfa na kushoto ni Mwenyekiti wa TUGHE, Obedi Mbaga.
Mkurugenzi
wa Idara ya Sheria katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Marlin Komba
akijitambulisha mbele ya Naibu Katibu Mkuu mpya, John Mngodo (hayupo pichani)
wakati wa Mkutano kati ya Watumishi na Naibu Katibu Mkuu huyo uliofanyika
katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara.
Naibu
Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, John Mngodo, akizungumza
na Watumishi mara baada ya kuanza kazi rasmi katika Wizara hiyo.
Watumishi
wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu mpya wa
Wizara (hayupo pichani) alipofanya mkutano na watumishi hao mara baada ya
kuanza kazi rasmi katika Wizara hiyo.(Picha
na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
Imeandaliwa na Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.