Mauaji katika mghahawa wa Rue Bichat, Paris Gari la huduma ya kwanza.Walionusulika katika shambulizi lililofamyika kwenye ukumbi wa Batclan. ...Wakiokolewa. Miili ya marehemu katika mhgahawa wa Cambodian.
Hali ya sintofahamu mjini paris.Kikosi cha uokoaji.
...Mmoja wa waliouawa baada ya kukutwa eneo la Boulevard des Filles du Calvaire karibu na Btclan, Paris. ...Wakiokolewa.Polisi wakikagua vitambulisho vya raia wakati wa doria.Eneo amabapo mashambulizi hayo yamefanyika
Hali ilivyokuwa uwanja wa michezo wa Ufaransa, Stade de France
Paris, Ufaransa
UFARANSA imetangaza hali ya hatari na
kufunga mipaka yake baada ya watu zaidi ya 150 kuuawa kwenye mashambulio
mjini Paris, usiku wa kuamkia leo.
Watu 118 wameuawa baada ya kuvamiwa,
kutekwa na baadaye kufyatuliwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa ni
wapiganaji wa IS katika ukumbi wa sanaa wa Bataclan, katikati mwa Mji wa
Paris wakati walipokuwa wakitazama tamasha.
Watu wenye silaha walishika mateka watu
waliokuwa kwenye ukumbi huo kabla ya maofisa wa polisi kufika meneo la
tukio na kupambana nao na kuwazidi nguvu.
Watu wengine waliuawa kwenye mlipuko
uliotokea karibu na uwanja wa michezo wa taifa hilo, Stade de France
ambako mechi ya kirafiki kati ya Ufaransa na Ujerumani ilikuwa
ikiendelea.
Viongozi wa Mji wa Paris wamewataka raia
kubaki majumbani mwao wakati wanajeshi 1500 wa nchi hiyo wameingia
katika mitaa mbalimbali ya mji wa Paris kufanya doria kuwasaka wahusika
wa mashambulizi hayo.
Shambulio baya zaidi linaonekana kuwa
hilo la Bataclan, ambako ripoti zinasema watu waliokuwa wamehudhuria
tamasha ukumbini walipigwa risasi na kuuawa baada ya kushikwa mateka.
Akiongea baada ya kufika katika ukumbi
huo baadaye, Rais wa Ufaransa Francois Hollande ameapa kuwa wahusika
watakabiliwa "bila huruma".
Mashambulio mengine yalitokea karibu na
mighahawa ya Le Petit Cambodge watu wapatao 11 wameuawa Rue Bichat,
Cambodian, na Le Carillon katika mtaa namba 10.
Rais wa Marekani Barack Obama amelitaja
shambulio hilo kuwa "jaribio lisilokubalika la kuhangaisha raia wasio na
hatia" na kuahidi kuisaidia Ufaransa kukabiliana na waliohusika.
"Hili si shambulio tu dhidi ya raia wa Ufaransa. Ni shambulio dhidi ya binadamu wote na maadili yetu ya pamoja," amesema.
Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron
amesema ameshtushwa sana na shambulio hilo na kuahidi kufanya "lolote
tunaloweza kufanya kusaidia."