MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Dec 10, 2015

Faiza: kivazi cha mwaka huu kitawapa presha

Faiza AllyMREMBO Faiza Ally, ambaye amejizolea umaarufu baada ya kutinga ukumbini akiwa amevaa ‘Pampers’ siku ya kuzaliwa kwake,amefunguka kuwa kivazi kingine akachokivaa Desemba 19, Fukwe za Coco Aqua kitawapa presha watu wengi kutokana na kuwa gumzo zaidi.
Akizungumza na kona ya Bongo Movies, Faiza ambaye ni mzazi mwenzake na Mbunge wa Mbeya Mjini,Joseph Mbilinyi alisema kuwa siku hiyo pia itakuwa siku yake ya kuzaliwa hivyo kivazi atakachokivaa hakijawahi kuvaliwa nchini.
“Pampers iliwashangaza watu lakini kwa kweli kivazi nitakachotinga safari hii hakijawahi kuvaliwa ulimwenguni kabisa.
Nitakuwa nikisherehekea siku yangu ya kuzaliwa na kutakuwa na kiingilio, fedha itakayopatikana nitawasaidia watoto yatima,” alisema Faiza.