Akizungumza na kona ya Bongo Movies, Faiza ambaye ni mzazi mwenzake na Mbunge wa Mbeya Mjini,Joseph Mbilinyi alisema kuwa siku hiyo pia itakuwa siku yake ya kuzaliwa hivyo kivazi atakachokivaa hakijawahi kuvaliwa nchini.
“Pampers iliwashangaza watu lakini kwa kweli kivazi nitakachotinga safari hii hakijawahi kuvaliwa ulimwenguni kabisa.
Nitakuwa nikisherehekea siku yangu ya kuzaliwa na kutakuwa na kiingilio, fedha itakayopatikana nitawasaidia watoto yatima,” alisema Faiza.