Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Samia Suluhu Hassan, na
Rais Mstaafu wa awamu ya Tano, Dkt. Jakaya Kikwete, wakiangalia moja ya
Ndege ya Kivita ya mfano, wakati walipotembelea Mabanda ya maonesho ya
Mkutano Mkuu wa Tano wa Wakuu wa Nchi za Afrika na China, uliofanyika
Jijini Johannesburg Afrika ya Kusini jana. Dkt. Jakaya Kikwete
alihudhuria mkutano huo kama Rais Mstaafu mwalikwa. Mkutano huo
unamalizika Dec 5, 2015.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan,
akiwa katika ukumbi wa mkutano wakati akijiandaa kuhutubia kwenye
Mkutano mkuu wa Tano wa Wakuu wa Nchi za Afrika na China, unaomalizika
leo jijini Johannesburg Afrika ya Kusini.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan,
akizungumza na Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Balozi Liberata Rutageruka Mulamula, kabla ya kuhutubia katika Mkutano
mkuu wa Tano wa Wakuu wa Nchi za Afrika na China, unaomalizika leo
jijini Johannesburg Afrika ya Kusini. Picha na OMR