Rais
Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
akibadilishana mawazo na Rais wa China, Mheshimiwa Xi Jinping pembezoni
mwa Mkutano wa Africa na China unaofanyika Johannesburg , Afrika
Kusini. Waliosimama pembeni ni Mhe. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais
wa Tanzania, Rais Thomas Boni Yayi wa Benin, Rais Filipe Nyusi wa
Msumbiji na Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini.
----------------------------------
Taasisi
ya Commonwealth Partnership for Technological Management (CPTM)
inayojishughulisha na kukuza ushirikiano katika nyanja ya sayansi na
teknolojia kwa nchi za Jumuiya ya Madola, imemtunuku Rais Mstaafu Jakaya
Mrisho Kikwete, heshima ya Juu ya CPTM (Companion Award) kwa kutambua
mchango wake katika kuhamasisha ukuaji wa matumizi ya sayansi na
teknolojia ikiwemo matumizi ya huduma za fedha kwa njia ya simu. Rais
Mstaafu Kikwete, alikabidhiwa Tuzo hiyo tarehe 1 Desemba, 2015.
Taasisi
hiyo yenye makao makuu yake London ndio inayoendesha Midahalo ya
Kimataifa maarufu kama Smart Partnership Dialogue. Mkutano wa mwisho wa
aina hiyo ulifanyika Dar es Salaam mwaka 2013 ukiwa Na kali mbiu ya
"Kutumia Teknolojia Kuchochea Maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii Barani
Afrika".
Rais
Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Cheti cha Kumtunuku
Yeshima ya Juu ya CPTM (Companion Award). Aliyesimama kushoto kwa Rais
Mstaafu ni Dkt. Tan Sri Omar, Mwenyekiti wa Bose ya Wakurugenzi wa CPTM
na pembeni yake ni Dkt. Mihaela Smith, CEO wa CPTM. Tuzo
hiyo imetolewa wakati wa Mkutano Mkuu wa 20 wa CPTM ambao uliambatana
na maadhimisho ya Miaka 20 ya Taasisi hiyo jijini London.Rais
Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akitoa neno la shukurani baada ya
kutunukiwa tuzo ya heshima ya Juu ya CPTM (Companion Award) wakati wa Mkutano Mkuu wa 20 wa CPTM ambao uliambatana na maadhimisho ya Miaka 20 ya Taasisi hiyo jijini London.
|
Rais
Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete aliteuliwa na Mama Nkosamana Dlamini
Zuma kuwa Mjumbe Maalum wa AU Comoro. Mhe. Kikwete alikwenda Moroni,
Comoro tarehe 30 Novemba, 2015 kufanya mikutano na wadau wa siasa kuhusu
mgogoro wa kisiasa unaonukia nchini humo kuhusu mchakato wa uchaguzi
mkuu wa nchi hiyo utakaofanyika April, 2016