Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Abednego Damian ‘Belle 9.
STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Abednego Damian ‘Belle 9’ amefungukia
ukimya wake uliojitokeza mwaka jana kuwa, kurudi kwake upya kwenye gemu
ya muziki kumesababishwa kwa kiasi kikubwa na Meneja wa Wasanii Bongo,
Hamis Taletale ‘Babu Tale’.Akichonga na Amani, Belle 9 anayebamba na Ngoma ya Burger, Movie, Selfie alisema Babu Tale alihusika kwa asilimia zote kumrudisha kwenye muziki na kumweka katika Lebo ya Vitamini Music ambayo yupo hadi sasa na kwamba bila msanii huyo ingemchukua muda mrefu kurudi kwenye gemu