MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

May 30, 2017

Uchumi umeyumba sana - Mzee Yusuf

Mzee Yusuf
 Aliyekuwa mmiliki wa band ya Jahazi Modern Taarab, Mzee Yusuf amefunguka na kusema toka ameamua kuachana na biashara ya muziki na kumrudia Mungu maisha yake yameyumba sana lakini amekuwa na amani, furaha na maisha hayo kuliko kipindi cha nyuma.
Mzee Yusuf amesema wakati anafanyakazi ya muziki alikuwa na maisha bora sana na kufanya vitu ambavyo anataka kufanya bila wasiwasi wowote tofauti na sasa ambapo akihitaji kitu fulani lazima ajipange kweli kweli ili kukipata.
"Maisha niliyonayo sasa ni maisha ambayo yana amani kuliko maisha niliyokuwa nayo huko nyuma, haya ni maisha ya utulivu kwa hilo nashukuru Mungu, lakini si yale maisha bora kama niliyokuwa nayo kipindi kile naweza kutaka pilau leo, biliani kesho napika lakini leo hii nikitaka biliani lazima nijipange, kwa hiyo uchumi kwangu umeyumba sana lakini nashukuru sina wasiwasi, yaani sina pressure katika maisha yangu" - alisisitiza Mzee Yusuf.