Miili ya Watu zaidi ya 230
wanaoelezwa kuawa na Wanamgambo wa Islamic State imepatikana katika
kaburi la pamoja mashariki mwa Syria, Wanaharakati wameeleza.Shirika la uangalizi wa haki za
binaadam la Syria limesema Watu hao wanakisiwa kuwa jamii ya kabila
moja lililokuwa likipambana na kundi la Jihad jimbo la Deir al-Zour.
Kaburi
la pamoja liligunduliwa baada ya Watu wa jamii ya kabila la Sheitat
kuruhusiwa na Viongozi wa Wanamgambo wa IS kurejea nyumbani.
Mwezi uliopita , Umoja wa Mataifa ulisema umepokea ripoti kuhusu mauaji mjini humo mwezi Agosti.
Wachunguzi
wanasema kuwa inaonyesha kuwa mauaji hayo yalitekelezwa na wanamgambo
wa Islamic State katika harakati ya kudhibiti rasilimali ya mafuta
karibu na Mji wa Mohassan.
Mmoja kati ya manusura amesema aliona
vichwa vingi vikiwa vimening'inizwa kwenye kuta, lakini yeye alifanikiwa
kutoroka na familia yake.
Mauaji yanaripotiwa kutokea baada ya
mazungumzo kati ya pande hizo mbili kuvunjika huku jamii ya kabila la
Sheitat ikikataa kutekeleza yale waliyokubaliana na IS.