Wanajeshi 54 wamehukumiwa adhabu ya
kifo na mahakama ya Kijeshi nchini Nigeria kwa kukataa kupambana na
Wanamgambo wa kiislamu, Boko Haram.
Wanajeshi walikutwa na hatia
ya uasi ,kushambulia na uoga.Wanajeshi hao wanashutumiwa kukataa
kupigana kurudisha miji mitatu iliyokuwa ikishikiliwa na Boko Haram
mwezi Agosti.Mwanasheria wa Wanajeshi hao amesema wamehukumiwa kifo cha kupigwa risasi na kikosi maalum huku Wanajeshi wengine watano wakiachiliwa.
Vikosi vya kijeshi vya Nigeria vimedai kuzidiwa silaha na Boko Haram, kwa kuwa hawapatiwi silaha za kutosha kupambana na Wanamgambo.
Boko Haram wanapambana kuunda himaya ya kiislamu kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.