MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Dec 24, 2014

DIAMOND APELEKA TUZO ZA CHANNEL O KWA JK

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete akiwa na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul  'Diamond Platnumz' baada ya kumtembelea leo Ikulu jijini Dar es Salaam.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo toka kwa msanii Naseeb Abdul “Diamond” wakati akimuonesha moja ya tuzo kati ya tuzo tano za muziki za kimataifa alizoshinda mwaka huu, Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Desemba 23, 2014. kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni Katika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Hermas Mwansoko.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na msanii Naseeb Abdul “Diamond” baada ya kumkaribisha na kumpongeza kwa kushinda tuzo tano za muziki za kimataifa mwaka huu, Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Desemba 23, 2014. Kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni Katika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Hermas Mwansoko, na kushoto ni katibu wa Bodi ya filamu Tanzania Bi. Joyce Fissoo.
Rais Dk. Jakaya Kikwete leo amewapongeza mwanamuziki Diamond Platinumz na mshindi wa shindano la Big Brother Hotshots Idris Sultan kwa ushindi walioupata hivi karibuni huko nchini Afrika Kusini.
Rais Kikwete amempongeza Diamond kwa kutwaa tuzo tatu za muziki za Channel O huku akimpongezza pia Idris kushinda BBA bila kufanya mambo machafu mjengoni.