Inasemekana penzi kati ya waigizaji Chuchu Hans na Visent Kigosi
“Ray” limeingia mtegoni baada ya Chuchu Hans kusemekana kumsaliti mpenzi
wake Ray kwa jamaa anayedaiwa kuwa ni mfanyabiashara anayeishi maeneo
ya Mbezi Beach Dar.
Chanzo kinasema pamoja na Chuchu kuwa na Ray kwa muda wote, lakini
inadaiwa kuwa muda fulani amekuwa akitoka na kwenda Mbezi anapoishi
kijana huyo.
Hata hivyo paparazi wetu aliamua kumvutia waya Chuchu na kuzungumza
naye ishu hiyo ambapo alidai stori hizo zinasambazwa na watu ambao lengo
ni kutaka kumchafua kwa mpenzi wake Ray.
“Watu hawapendi kuniona natoka na Ray na ni hao ndiyo wanaotumia muda
mwingi kutaka kutuvuruga. Siwezi kufanya hivi na huyo jamaa sijui wa
Mbezi kwanza simfahamu na pili jamii haitanielewa nikifanya hivi,”
alisema Chuchu.
Stori na Laurent Samatta
BONGO MOVIE