Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Margaret Zziwa aondolewa
madarakani na wabunge wa Afrika Mashariki na Kumpa saa 24 kukabidhi
ofisi hii imekuja baada ya Wabunge wenzake kupiga kura za kutokuwa na
imani naye. Bunge la Afrika Mashariki (EALA), limeidhinisha
kumuondoa madarakani Spika wa Bunge hilo Mhe. Margaret Zziwa anayetokea
Uganda kwa tuhuma za kutumia vibaya madaraka, kutumia vibaya ofisi ya
spika pamoja na kutowaheshima wajumbe wa bunge hilo.
Hatua hiyo inafu
atia ripoti ya Kamati ya Kanuni na Sheria ya EALA, iliyomtia hatiani Mhe Zziwa na kuridhia kuwajibika mara moja.
Katika kikao hicho kilichokuwa chini ya Mwenyekiti Chris Opoka, ambaye
ni Spika wa muda, kura 36 kati ya 39 zilizopigwa na wajumbe wa bunge
hilo waliokuwepo walipitisha hoja ya kumvua madaraka Mhe. Zziwa.