Serikali
imesema uchaguzi wa Serikali za Mitaa
uliofanyika jana Kote Nchini umefanikiwa kwa Zaidi ya asilimia 98% katika Mikoa
yote .
Hayo
yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa (TAMISEMI) Hawa Ghasia wakati wa mkutano na waandishi wa Habari leo
jijini Dar es salaam uliolenga kutoa ufafanuzi kuhusu mafanikio ya uchaguzi
huo.
Akifafanua
Mh. Ghasia amesema kwa kiwango kikubwa wananchi walijitokeza kupiga kura na
kuchagua viongozi wao katika ngazi ya Mitaa,Vijiji, na Vitongoji. Akizungumzia
mafanikio ya Uchaguzi huo Mh. Ghasia
alitaja Mikoa ambayo uchaguzi umefanyika katika Halmashauri na Kata zote kuwa
ni Arusha,Mbeya,Kagera,Njombe,Singida,Lindi,Ruvuma,Katavi na Geita.
Mikoa
Mingine iliyofanya vizuri katika uchaguzi huo ni Iringa,Dodoma,Mtawara ambapo
Mh. Ghasia aliwapongeza Viongozi na wataendaji wote wa Mikoa na Halmashauri
hizo pamoja na wananchi kwa kazi kubwa na nzuri waliyofanya hadi kufanikisha
uchaguzi huo.
Akitoa
ufafanuzi Zaidi kuhusu maboresho yaliyofanywa na Serikali katika uchaguzi huo
Mh. Ghasia amesema kuwa mojawapo ni kuwepo kwa utaratibu wa kupiga kura kwa
kutumia karatasi maalum zilizochapishwa kitu ambacho katika uchaguzi uliopita
hakikuwepo.
Akizungumzia
Mikoa ambayo baadhi ya Halmashauri zimeahirisha uchaguzi ama Halmashauri yote
au sehemu ya Kata zake kwa sababu mbalimbali ikiwemo kuchelewa kufika kwa vifaa
vya kupigia kura Mh.Ghasia aliitaja kuwa ni Kilimanjaro katika Halmashauri ya
Wilaya ya Rombo na Hai,Manyara katika Halmashauri za Hanang na mbulu.
Mikoa
Mingine ni Morogoro katika Halmashuri ya Wilaya ya Ulanga na Mvomero,Mkoa wa
Shinyanga Halmashauri ya Wilaya ya Msalala,Mkoa wa Simiyu Halmashauri ya Wilaya
ya Busega na Itilima ambapo Mikoa mingine ambayo kasoro ndogondogo zilijitokeza
na kupelekea uchaguzi kuahirishwa katika baadhi ya Kata ni
Kigoma,Mwanza,Tabora,Tanga,Mara,Rukwa,Pwani na Dar es salaam.
Akizungumzia Hatua zitakazochukuliwa na Serikali
kufuatia dosari zilizojitokeza.