MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Jan 12, 2015

Vita vipya dhidi ya waasi wa FDLR

Serikali ya Angola inasema kuwa uamuzi umechukuliwa na mataifa ya Afrika kuingilia kijeshi harakati za waasi wa kihutu kutenda uhalifu Mashariki mwa Congo.
Afisaa mmoja mkuu (Joaquim do Espirito Santo) anasema kuwa mkutano wa kikanda uliotarajiwa kufanyika leo, umefutiliwa mbali kwa sababu ya hofu ya kuchelewesha mipango ya kijeshi dhidi ya waasi hao.
Umoja wa mataifa ulithibitisha mwishoni mwa wiki jana kwamba waasi wa FDLR wamepitwa na muda waliowekewa wa mwisho kwao kusalimisha silaha.
Wiki jana Rais wa DRC, Joseph Kabila, aliambia katibu mkuu wa umoja wa Mataifa kuwa jeshi la nchi yake liko tayari kupambana na waasi hao.
Mkuu wa kikosi cha kulinda amani cha umoja wa Mataifa, (Martin Kobler) amesema kuwa hatua za kijeshi ndizo pekee zinahitajika kuchukuliwa dhidi ya waasi hao kwa sasa.