Uchunguzi huo umebaini kwamba moja ya makampuni yaliyositisha mikataba ya wasanii ni Steps Entertainment ambao wamesababisha mastaa kibao kushindwa kutengeneza muvi kwa kuwa awali walikuwa wakipewa bajeti na Steps kisha kuwauzia kwa bei ya mapatano.
Ilibainika kwamba baada ya Steps kuachana na utaratibu huo na kudai kuwa wanachukua muvi zilizoandaliwa na makampuni binafsi za mastaa wachache kama Jacob Steven ‘JB’, Athuman Amri ‘Mzee Majuto’, Vincent Kigosi ‘Ray’ na wengine wenye makampuni binafsi.
Mmoja wa mastaa wakubwa wa filamu, Musa Issa ‘Cloud 112’ alikiri kuwepo kwa hali hiyo huku akifafanua kuwa Steps kuna wakati inakuwa kwenye kipindi kigumu.
Wewe kama mdau una maoni gani juu ya hili.