MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Apr 11, 2015

Rais Mstaafu Mkapa atoa elimu ya uchumi kwa Mabalozi, maofisa na wafanyakazi Wizara ya Mambo ya Nje

  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb) akimpokea Rais wa awamu ya tatu Mhe. Benjamin William Mkapa mara baada ya kuwasili Mwalimu Nyerere kwa ajili ya semina hiyo. 
 Rais Mstaafu Mkapa akiteta jambo na Mhe. Membe wakati wa semina hiyo ambapo alizungumzia changamoto za ushirikiano wa kiuchumi na diplomasia nchini Tanzania, na nje ya nchi na Jumuiya za Kimataifa. Andiko la mada hii litapatikana baada ya muda mfupi kwenye tovuti ya Wizara.

 Mabalozi, Maofisa na Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje pamoja na Walimu na Wanachuo cha Diplomasia wakimsikiliza kwa makini Mhe. Benjamin W. Mkapa.
 Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Benjamin William Mkapa akitoa mada katika semina ya masuala ya diplomasia ya kiuchumi kwa Mabalozi, Maofisa na Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa (hawapo pichani). Semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere jijini Dar es Salaam tarehe 9 Aprili 2015.
 Mabalozi, Maofisa na Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje pamoja na Walimu na Wanachuo cha Diplomasia wakimsikiliza kwa makini Mhe. Benjamin W. Mkapa.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali kwa Umma wa Wizara ya Mambo ya Nje Bi. Mindi Kasiga akiuliza swali kufuatia mada iliyotolewa na Rais Mstaafu Mhe. Mkapa katika hiyo semina hiyo.
 
na michuzi media/babu wambura