Kampuni ya mawasiliano ya Airtel Tanzania
kupitia mtaji wake wa Airtel Fursa “Tunakuwezesha”* imeendesha semina ya
mafunzo ya biashara kwa vijana wenye umri kati ya miaka 18-24 mwishoni
mwa wiki hii kwa ajili ya kutoa ujuzi na mbinu za kumbambana na
changamoto za biashara na jinsi ya kuendesha biashara zao katika ukumbi
wa Golden Rose Mjini Arusha.
Vijana wengi waliweza kuhudhuria semina
hiyo ambayo iliwapo mafunzo ambayo yataweza kuwasiadia katika kutatua
changamoto wanazokutana nazo katika maisha yao ya kila siku na katika
ulimwengu wa sasa wenye ushindani mkubwa wa biashara.
Airtel, Kupitia mradi wake wa *Airtel Fursa
“Tunakuwezesha”* umewawezesha vijana zaidi ya mia mbili kupata mafunzo
ya biashara na pia wengine kubahatika kwa kuwezeshwa na vitendea kazi
vya kuinua biashara zao. Mikoa ambayo imeweza kuwezeshwa mpaka sasa ni
Dar Es Salaam, Mwanza na Arusha na wiki ijayo wakaai wa Mtwara
watawezeshwa.
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel
Tanzania, Beatrice Singano Mallya alisema “Tunajivunia kudhamini semina
hii kwa kuwa moja ya dhamira ya kampuni yetu ni kuwawezesha vijana hapa
nchini kwa namna mbalimbali ikiwemo
kuwapatia maarifa na ujuzi kama ambavyo katika semina hii wameweza kupata mbinu za kuendesha biashara zao na tunaamini wakizitumia wataweza kupata mafanikio na maisha yao kuwa murua.”
kuwapatia maarifa na ujuzi kama ambavyo katika semina hii wameweza kupata mbinu za kuendesha biashara zao na tunaamini wakizitumia wataweza kupata mafanikio na maisha yao kuwa murua.”
Aliongeza kuwa Tanzania kama zilivyo nchi
nyingine imekuwa ikikabiliwa na tatizo la ajira hususani kwa vijana.
Kukosa mbinu za kupata mikopo, na ushindani mkubwa uliopo kwenye soko la
biashara.”Mafunzo haya ni muhimu na yanaenda sambamba na utekelezaji wa
malengo ya kuwainua wajasiriamali ili kuweza kuwainua vijana hapa
nchini,” alisema.
Baadhi ya vijana waliohudhuria semina hiyo
waliishukuru Airtel kwa kuandaa semina ya kutoa ujuzi wa baishara katika
nyanja mbalimbali.
”Tumeweza kupata maarifa na tunawashukuru
sana Airtel kwa kufanikisha kuwepo semina hii. Kuna vijana wengi sana
huko mtaani ambao hawajui pakuanzia ili kupata elimu ya kuinua biashara
zao. Lakini leo hii, Airtel imeona umuhimu wetu na kuamua kutuwezesha
kwa kutupatia mafunzo haya muhimu,” alisema Bi Naima Aboubakar mmoja wa
washiriki kwa niaba ya wenzake