
Mkurugenzi
wa Elimu ya juu kutoka Wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi Stadi,
Prof. Sylivia Temu (katikati waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na
uongozi wa chuoChuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha
Muhimbili (MUHAS), wawakilishi kutokakutoka Benki ya Maendeleo ya
Afrika (AfDB) pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya afya baada
yauzinduzi
mradi wa ujenzi wa kituo cha ubora wa sayansi ya magonjwa na mishipa ya
moyo hapa nchini uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kituo hicho
kitakachokuwa na uwezo wa kutoa huduma za kitabibu na kitafiti kwenye
magonjwa hayo kwa nchi zote za ukanda wa Afrika mashariki na kitakuwa
chini ya usimamizi wa (MUHAS).


Na Mwandishi wetu,
SERIKALI
imezindua mradi wa ujenzi wa kituo cha ubora wa sayansi ya magonjwa na
mishipa ya moyo hapa nchini kitakachokuwa na uwezo wa kutoa huduma za
kitabibu na kitafiti kwenye magonjwa hayo kwa nchi zote za ukanda wa
Afrika mashariki.
Akizungumza
wakati wa uzinduzi wa mradi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam jana
kwa niaba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi stadi Bw. Shukuru
Kawambwa, Mkurugenzi wa Elimu ya juu nchini, Prof. Sylivia Temu alisema
mradi huo unaotekelezwa na serikali kwa ushirikiano na benki ya
maendeleo ya Afrika ni
mojawapo ya miradi minne ya afya inayotekelezwa kwenye ukanda wa afrika
mashariki ikilenga kutatua changamoto mbalimbali za kiafya.