MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Sep 9, 2015

UMEME WA PUMBA ZA MCHELE, MASHUDU YA PAMBA WATUMIKA KUENDESHEA MITAMBO YA TBL MWANZA

 Meneja wa kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Mwanza, Raymond Richmond,akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kampuni hiyo  kutumia mapumba ya mchele na mashudu ya pamba,kama chanzo cha nishati ya umeme kinachotumika kuendeshea mitambo.Kushoto ni Meneja wa Maji na Nishati wa kampuni hiyo, Sunday Kidolezi.
Meneja wa kiwanda cha Kampuni ya Bia (TBL) Mwanza, Raymond Richmond, akizungumzia mradi wa matumizi ya mapumba ya mchele na mashudu ya pamba,ambacho ni chanzo cha nishati ya kuendesha mitambo kiwandani hapo.Nishati ni rafiki wa mazingira  kwa sababu haina hewa ukaa.Wanaokoa Dola za Kimarekani (USD) 400,000 hadi 500,000 kwa mwaka ambazo zingetumika kununua mafuta mazito na dizeli ya kuendeshea mitambo .
Waandishi wa habari wakiongozwa na  Meneja wa Kiwanda cha kampuni ya Bia (TBL) Mwanza, Raymond Richmond(wa kwanza kushoto), kwenda kutembelea mtambo unaotumia mapumba ya mchele na mashudu ya pamba kuzalisha nishati ya umeme inyotumika kuendesha mitambo ya kiwanda hicho.Kulia ni Meneja wa Maji na Nishati wa TBL, Sunday Kidolezi.