MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Nov 27, 2015

DC AAGIZA MUUGUZI ALIYEKAMATWA KWA WIZI WA DAWA SHINYANGA ASIMAMISHWE KAZI MARA MOJA,

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amefanya ziara ya kushtukiza katika kituo cha afya Kambarage mjini Shinyanga ili kujionea hali halisi jinsi huduma zinavyotolewa kwa wananchi siku moja tu baada ya muuguzi wa kituo hicho kukamatwa kwa tuhuma ya kuiba dawa za serikali.Pichani ni mkuu wa wilaya Josephine Matiro na katibu tawala wa wilaya ya Shinyanga wakiwa katika chumba cha kuhifadhia dawa wakiwa wamepigwa butwaa baada ya kuona chumba kimesheheni dawa wakati mara kwa mara wananchi wamekuwa wakiambiwa hakuna dawa badala yake wanaambiwa wakanunue kwenye maduka ya watu binafsi mtaani-Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog . Hapa ni ndani ya ofisi ya mganga mkuu/msimamizi wa kituo hicho ambapo mkuu wa wilaya akiwa ameambatana na maafisa wengine wa manispaa ya Shinyanga amekutana na uongozi wa kituo hicho pamoja na wananchi waliomkamata muuguzi mkunga wa kituo hicho Joseph Nkila akituhumiwa kuiba dawa za serikali.Kulia ni Rashid Shaban akimweleza mkuu huyo wa wilaya jinsi walivyofanikisha kufichua wizi huo Wa pili kutoka kulia ni msimamizi wa kituo cha afya Kambarage Dkt Nassoro Yahya akitoa maelezo kwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga kuhusu suala la upungufu wa dawa katika kituo chake ambapo alisema kituo kina upungufu wa dawa na walishatoa taarifa panapohusika siku nyingi zilizopita.Hata hivyo maelezo yake yalipingana na yale ya kaimu mganga mkuu wa manispaa ya Shinyanga Dkt Mhana Raphael(mwenye suti pichani) aliyedai kuwa mkoa wa Shinyanga hauna tatizo la upungufu wa dawa bali dawa pekee ambayo haipo ni ile ya Antibiotic Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza katika kituo cha afya cha Kambarage mjini Shinyanga ambapo pamoja na mambo mengine amemwagiza mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga kumsimamisha kazi muuguzi Joseph Nkila anayetuhumiwa kuiba dawa za serikali pamoja na msimamizi wa kituo hicho Dkt Nassoro Yahya kwa uzembe unaosababisha mwanya wa upotevu wa dawa katika kituo hicho na kusababisha wananchi kuilalamikia serikali kwa kukosa dawa wakati mkoa wa Shinyanga hauna tatizo la dawa