Mkuu
wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia
Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues akitoa
neno la ufunguzi katika mkutano huo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi
kufungua.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof. Ole Sante
Gabriel akisisitiza jambo wakati akifungua rasmi mkutano wa kitaifa wa
mashauriano kuhusu hali ya usalama wa waandishi wa habari, uzinduzi wa
kikosi kazi cha usalama wa waandishi wa habari na uandishi unaozingatia
maadili ambao umeandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na
Elimu, Sayansi (UNESCO).
Makamu wa Rais wa Chama cha Kijamii cha Wanasheria wa Tanganyika, Bi. Flaviana Charles akifafanua jambo wakati wa mkutano huo.
Mhadhiri
wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) katika tasnia ya Habari na
Mawasiliano, Ayub Rioba akiwasilisha mada ya wajibu wa vyombo vya habari
huku akitolea mfano wa moja ya habari iliyobeba kichwa cha habari
"Uhuru wa habari watikiswa Zimbabwe" katika moja ya magazeti ya Serikali
wakati wa mkutano wa kitaifa wa mashauriano kuhusu hali ya usalama wa
waandishi wa habari, uzinduzi wa kikosi kazi cha usalama wa waandishi wa
habari na uandishi unaozingatia maadili ulioandaliwa na UNESCO.
Mkurugenzi
wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene akitolea ufafanuzi wa
swali la Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima, Neville Meena
(hayupo pichani).
Ofisa
Miradi katika kitengo cha Mawasiliano na Tehama UNESCO, Nancy Kaizilege
akiwasilisha mada ya Uhuru wa vyombo vya Habari katika mkutano huo.
Mkuu
wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia
Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues
(katikati) akisalimiana na Mjumbe wa bodi udhamini ya Mtandao wa Radio
Jamii Tanzania (COMNETA), Balozi Mstaafu, Christopher Liundi alipowasili
katika mkutano wa kitaifa wa mashauriano kuhusu hali ya usalama wa
waandishi wa habari, uzinduzi wa kikosi kazi cha usalama wa waandishi wa
habari na uandishi unaozingatia maadili ulioandaliwa na UNESCO. Kulia
ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof.
Ole Sante Gabriel.