Kova amesema hayo leo alipokuwa akizungumza katika kipindi cha kumekucha cha ITV, ambapo amesema mkataba wake na jeshi la Polisi umeishia leo, hivyo analazimika kukaa pembeni katika kuitumikia jeshi hilo.
“Mmepata bahati sana, maana wakati nakuja Dar es salaam mwaka 2008 nikitokea Mbeya, kwa mara ya kwanza nilifanya kipindi hapa na leo hii nawaagia hapa, leo ndio siku ya mwisho kwangu kulitumikia jeshi la Polisi, mkataba wangu na jeshi la Polisi unaisha leo, lakini siwaachi hivi hivi, Kaimu wangu yupo atakuwa nanyi”, alisema Kamanda Kova.