Waziri
wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhe.Profesa Makame Mbarawa akitoa
maelezeko ya utendaji kwa Naibu Mkurugenzi wa TAZARA Bw. Betram Kiswaga
alipotembelea Ofisi za Shirika hilo leo jijini Dar es salaam.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe.Profesa Makame Mbarawa akiongea
na Viongozi pamoja na Wafanyakazi wa TAZARA alipotembelea ili kutoa
muongozo wa utendaji kazi katika Shirika hilo.
1. Wafanyakazi wa Shirika la TAZARA Wakimsikiliza Waziri Profesa Mbarawa (Hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame mbarawa amewataka
watendaji na wafanyakazi wote wa shirika la reli la Tanzania na Zambia
(TAZARA), kufanya kazi kwa umoja,uwazi na uadilifu ili kufikia malengo
yaliokusudiwa na kuhuisha ustawi wa shirika hilo.
Akitoa
mwelekeo wa utendaji wa shirika hilo kwa watendaji na watumishi wa
TAZARA Prof. Mbarawa amesema Serikali ya awamu ya tano inaitaka TAZARA
kufanya kazi kibiashara kwa kuhudumia wasafiri na wasafirishaji
kikamilifu ili kuinua uchumi wa shirika hilo na kuliondolea unyonge na
migogoro ya mara kwa mara.
“Acheni
kufanyakazi kwa upendeleo na usiri kwani huo ndio mwanzo wa hujuma na
ubadhirifu hali inayochochea malalamiko na kudumaza TAZARA”, amesema
Prof. Mbarawa.Amezungumzia
umuhimu wa kila mfanyakazi kufanya kazi kwa uadilifu na malengo ili
kuleta matokeo chanya kwa manufaa ya TAZARA na nchi wanachama.
Kuhusu ubadhirifu unaotokea TAZARA Prof. Mbarawa uchunguzi wa TAKUKURU umeshaanza na kusisitiza kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wahalifu wote bila kujali wanatoka upande gani wa TAZARA. Naibu
Mkurugenzi wa TAZARA Bw, Betram Kiswaga amemweleza Waziri kuwa TAZARA
inakabiliwa na changamoto za kimtaji,kiufundi na upungufu wa injini na
mabehewa hivyo ameiomba serikali kuiwezesha ili imudu kujiendesha.
Amemhakikishia
Waziri kuwa tayari shirika hilo limeanza kupata wasafirishaji wa
uhakika hivyo kuimarika kimtaji kutavutia wasafirishaji wengi zaidi.Reli
ya TAZARA inayounganisha nchi za Tanzania na Zambia iliyojengwa na
wachina miaka ya sabini na ina mtandao wa KM 1860 kutoka Dar es Salaam
hadi Kapirimposhi lengo likiwa ni kuimarisha biashara na uchukuzi kati
ya nchi hizo na kukuza uchumi.Imetayarishwa na Kitengo cha Habari, Mawasiliano Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.