MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Jan 6, 2016

Waziri Prof. Mbarawa asisitiza uwazi na uadilifu TAZARA

Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano  Mhe.Profesa  Makame Mbarawa akitoa maelezeko ya utendaji kwa Naibu Mkurugenzi wa TAZARA  Bw. Betram Kiswaga alipotembelea Ofisi za Shirika hilo leo jijini Dar es salaam.
   Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe.Profesa  Makame Mbarawa akiongea na Viongozi pamoja na Wafanyakazi wa  TAZARA  alipotembelea ili kutoa muongozo wa utendaji kazi katika Shirika hilo.
1.   Wafanyakazi wa Shirika la TAZARA Wakimsikiliza Waziri  Profesa Mbarawa (Hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame mbarawa amewataka watendaji na wafanyakazi wote wa shirika la reli la Tanzania na Zambia (TAZARA), kufanya kazi kwa umoja,uwazi na uadilifu ili kufikia malengo yaliokusudiwa na kuhuisha ustawi wa shirika hilo.

Akitoa mwelekeo wa utendaji wa shirika hilo kwa watendaji na watumishi wa TAZARA Prof. Mbarawa amesema Serikali ya awamu ya tano inaitaka TAZARA kufanya kazi kibiashara kwa kuhudumia wasafiri na wasafirishaji kikamilifu ili kuinua uchumi wa shirika hilo na kuliondolea unyonge na migogoro ya mara kwa mara.

“Acheni  kufanyakazi kwa upendeleo na usiri kwani huo ndio mwanzo wa hujuma na ubadhirifu hali inayochochea malalamiko na kudumaza TAZARA”, amesema Prof. Mbarawa.Amezungumzia umuhimu wa kila mfanyakazi kufanya kazi kwa uadilifu na malengo ili kuleta matokeo chanya kwa manufaa ya TAZARA na nchi wanachama.

Kuhusu ubadhirifu unaotokea TAZARA Prof. Mbarawa uchunguzi wa TAKUKURU umeshaanza  na kusisitiza kuwa hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wahalifu wote bila kujali wanatoka upande gani wa TAZARA. Naibu Mkurugenzi wa TAZARA Bw, Betram Kiswaga amemweleza Waziri kuwa TAZARA inakabiliwa na changamoto za kimtaji,kiufundi na upungufu wa injini na mabehewa hivyo ameiomba serikali kuiwezesha ili imudu kujiendesha.

Amemhakikishia Waziri kuwa tayari shirika hilo limeanza kupata wasafirishaji wa uhakika hivyo kuimarika kimtaji kutavutia wasafirishaji wengi zaidi.Reli ya TAZARA inayounganisha nchi za Tanzania na Zambia iliyojengwa na wachina  miaka ya sabini na ina mtandao wa KM 1860 kutoka Dar es Salaam hadi Kapirimposhi lengo likiwa ni kuimarisha biashara na uchukuzi kati ya nchi hizo na kukuza uchumi.Imetayarishwa na Kitengo cha Habari, Mawasiliano Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.