MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Oct 8, 2016

DC MJEMA AKUTANA NA WAJUMBE WA BARAZA LA ARDHI

  

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema amekutana na wajumbe wa baraza la ardhi la wilaya hiyo na kupanga mikakati ya kutatua migogoro katika kata mbalimbali.

Akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake jana Mjema alisema kuwa kuanzia sasa ataanza kuzunguka na wajumbe hao wa baraza katika kata mbalimbali ili waweze kujionea kwa macho tatizo la migogoro ya ardhi linalo wakabili.

“Hiki ni kikao cha kawaida tu chenye lengo la kupanga mipango mbalimbali ya kutatua changamoto zinazo wakabili wakazi wa Ilala haswa Migogoro ya ardhi” anasema Dc Mjema

Alisema lengo la ziara ni pamoja na kujenga mshikamano wa kikazi baina ya wananchi na Watendaji wa Serikali katika kutatua kero zao.
 
chanzo: Na Humphrey Shao, Blog ya Jamii