MY ADVERT EA SHOWBIZ

MY ADVERT EA SHOWBIZ

SIX OFFICE SOLUTION

MOCHRISPO

DARDY FASHION

Jan 8, 2015

Odama:Ndoa Haitanifanya Niache Filamu

Mwigizaji wa  filamu za Kibongo Jennifer Kyaka ‘Odama’, amedai kuwa mwanaume ambaye anaweza kumuoa jambo la kwanza lazima atambue kuwa yeye anafanya filamu kwa muda mrefu hivyo hawezi kuacha kazi yake kwa sababu ya kuingia kwenye ndoa.
Odama alifungua kinywa chake baada ya kuzungumza na paparazzi wa GPL, ambapo alidai kuwa haiwezi kutokea kuacha kufanya filamu ili amridhishe mwanaume kwani maisha yake yamekuwa yakiendeshwa na kazi hiyo kwa muda mrefu.
“Naamini kuwa yule ambaye atakuja kwa nia ya kunioa kwanza lazima atambue kuwa nafanya filamu, sitahitaji anieleze jambo la kuacha kazi yangu, mimi ni mwanamke ambaye nahitaji kupata maendeleo kupitia kazi zangu,” alisema.
Picha:Odama akiwa na mtoto wake.

BONGO MOVIES.COM