Mwigulu
Nchemba akiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mh:Simbachawene
wakikagua eneo la machinjio ya Vingunguti kabla ya kuzungumza na wadau
wa eneo hilo pamoja na uongozi wake.
Mh:Mwigulu Nchemba akiwa ameongozana na Mh:Simbachawene wakielekea kuzungumza na wananchi wanaotumia Machinjio ya vingunguti.
Mawaziri
kutoka kulia ni Naibu waziri wa Afya Mh:Kigwangallah,Wa pili kutoka
kulia ni Mbunge wa Jimbo la Segerea Mh:Bonah,Watatu kutoka kulia ni
Mh:Simbachawene na wa mwisho kushoto ni Mh:Mwigulu Nchemba wakijadiliana
jambo.
Mkutano ukiendelea wa kutoa majawabu kuhusu changamoto za Machinjioya Vingunguti.
Mh:Simbachawene
akiwaagiza watumishi wote wa Machinjio ya Vingunguti kuripoti ofisini
kwake Jumanne wakiwa na mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala.
Mh:Mwigulu
Nchemba akizungumza na Wananchi(Wadau) wa machinjio ya Vingunguti
kuhusu hatua za kinidhamu alizozichukua kwa Mkuu wa mnada wa pugu
inakotoka mifugo kabla ya kufika Machinjio ya Vingunguti kwa upotevu wa
mamilioni ya shilingi ya kodi za serikali.
Mawaziri wakiagana na wananchi mara baada ya mkutano wa kutatua kero zao za Machinjio kumalizika.
Furaha
ya Wananchi mara baada ya kutatuliwa kero zao kwa hatua za
awali,wananchi wanasukuma gari la Mh:Mwigulu Nchemba kama ishara ya
kukubali hatua alizochukua.
Mh:Mwigulu
Nchemba akiwa ameambatana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI
Mh:Simbachawene wakiwasili kwenye eneo la machinjio ya Vingunguti
kwaajili ya kutoa majawabu kutokana na kero mbalimbali zinazowakabili
wadau wa machinjio hayo.